Pages

Wednesday, September 4, 2013

KUMBUKUMBU ZA KIKAO CHA WANAMAPAMBANO KILICHOFANYIKA TAREHE 25/18/2013, BULL’S PARK SURVEY

WALIOHUDHURIA
  1. Wakati Kabaka
  2. Adam Millinga
  3. Godlisten Anderson
  4. Freddy Kyara
  5. Davis Kawa
  6. Elizabeth Samson
  7. Gemima Mabula
  8. Willehadi Akaro
Kikao kilianza saa 9 :45 alasiri na kufunguliwa na Mwenyekiti, Ndugu Wakati Kabaka.
AJENDA
  1. Usajili wa kikundi
  2. Taarifa ya fedha
  3. Taarifa ya matukio yaliyopita
  4. Katiba
  5. Mengineyo

1.       USAJILI WA KIKUNDI
Nyaraka zote muhimu zinazohitajika kwa ajili ya uandikishwaji ziko tayari, imebaki kupata barua toka kwa ofisi ya Mkuu wa Wilaya/Mkoa kwa uthibitisho
2.       TAARIFA YA FEDHA
Wajumbe walisomewa taarifa ya makusanyo na matumizi ya fedha zilizokusanywa tokea mwanzo wa kikundi.

Pia wajumbe walitoa wazo la kupanga upya tarehe ya kuanza kukusanya michango ya mwezi, ili kuwapa wajumbe ambao walichelewa kujiunga fursa ya kuwa na mzigo mdogo wa madeni ili kuweza kukamilisha jumla ya michango yote ambayo angetakiwa awe ametoa. Hivyo basi tarehe ya mwanzo iliamuliwa iwe ni mwezi wa kwanza mwaka 2013.(Januari, 2013.

3.       TAARIFA YA MATUKIO YALIYOTOKEA
Kulikuwa na baadhi ya matukio kwa wanamapambano 1999 na kama marafiki wajumbe waliwatembelea ili kuwajulia hali. Jumla ya michango ilikuwa ni shilingi 440,000/ - na iligawanywa kwa wajumbe waliotembelewa kama pole/faraja.
a)       Rabiel (Jimmy) Masue kupata ajali alipokuwa safarini kuelekea Mwanza. Kwa sasa anaelendelea vizuri na bado amelazwa katika hospitali ya Muhimbili, taasisi ya MOI, PRIVATE WARD – G.
b)       Celina Fernandes aliyefanyiwa operation. Kwa sasa anaendelea vizuri, yeye na mtoto na yupo nyumbani.
c)       Cecilia Simba aliyefiwa na baba mlezi.
Wajumbe wamepanga pia kwenda kuwatembelea Erasto Mavika na Balaja Mbogoma, ambao wamebahatika kupata watoto pia.
4.       KATIBA
Wajumbe wameona kuna umuhimu wa kuipitia katiba ya kikundi upya na kufanya marekebisho wa baadhi ya sehemu zinazotakiwa.
5.       MENGINEYO
Kulikuwa na taarifa za matukio mbalimbali kama ifuatavyo:
a)       Send off ya Mwanazali Mmevela inayotarajiwa kuwa tarehe 10/09/2013
b)       Ndoa ya Wakati Kabaka inayotarajiwa kuwa tarehe 01/11/2013
Adam Millinga aliombwa na Wakati kukusanya/kupokea michango ya wanamapambano.
c)       Ndoa ya ya Kudra Mbarouk inayotarajiwa kuwa tarehe 24/10/2013

Pia wajumbe walipanga kufanya “barbecue day” siku ya jumamosi ya mwisho ya mwezi wa tisa (9) na kwa makadirio yaliyofanywa, kila mjumbe atatakiwa kutoa shilingi elfu ishirini (20,000/-) . Eneo la tukio litatangazwa baadaye.
 Kikao kilifungwa na Mwenyekiti saa 11:00 jioni. Kikao kijacho kitafanyika tarehe 29/09/2013.


No comments:

Post a Comment